• Call us: +255 755 446 540
  • Email: info@tecden.or.tz
Tanzania Early Childhood Development Network (TECDEN)
SUPPORT US
  • Home
  • Who We Are
    • Overview
    • Constitution
    • Vision and Mission
    • Strategic Plans
    • Our Partners
    • Our Team
  • Our Work
  • Members
  • News & Resources
    • News and Events
    • Conferences
    • Reports and Publications
    • success stories
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
  • Contact Us

Serikali na Wadau Waja na Elimu Juu ya Corona kwa Watoto

  /   News and Resources   /   Serikali na Wadau Waja na Elimu Juu ya Corona kwa Watoto
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania (TECDEN) Bruno Ghumpi (mwenye shati la batiki) akitoa maelezo kuhusu umuhimu wa uwepo wa elimu kwa wazazi na walezi ili kuwaelimisha watoto kuhusu kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona katika kikao kilichofanyika jijini
Apr 08, 2020
Serikali na Wadau Waja na Elimu Juu ya Corona kwa Watoto
08Apr

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa kushirikiana na Mtandao wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania (TECDEN), Taasisi ya Chakula na Lishe, Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF) wameandaa mkakati wa kufikisha ujumbe kwa watoto kuhusu kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona.

Akizungumza leo katika kikao kazi kilichowakutanisha wadau hao jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania (TECDEN) Bruno Ghumpi amesema kumekuwepo na ujumbe mbalimbali katika kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona ila kumekosekana ujumbe maalum unaolenga makundi maaalum ikiwemo wanawake wajawazito na watoto wadogo kuanzia miaka 0 hadi minane.

Ameongeza kuwa kuwepo kwa elimu sahihi kwa watoto hao kuhusu ugonjwa wa COVID 19 itawasaidia wazazi au walezi na watoto wenyewe kupata taarifa zitakaziwasaidia kujikinga na Virusi hivyo ili kupunguza au kuondokana na maambukizi ya Virusi hivyo katika maeneo yao.

“Ujumbe huu kwa watoto ni muhimu sana kwani kundi hili kwa sasa lipo nyumbani kutokana na kufungwa kwa shule hivyo ni vizuri wazazi na walezi wakazingatia masuala muhimu ya kuwafundisha watoto wao kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona” amesema

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bw. Mathias Haule amesema kuwa ni muhimu kwa wadau kuhakikisha wanafikisha elimu katika ngazi ya chini kuanzia familia, kijiji/mtaa ili kuwezesha watu hao kupata taarifa na elimu sahihi juu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.

“Elimu ifike katika ngazi ya familia hasa katika maeneo ya vijijini ambako bado elimu haijawafikia kwa kasi inayotakiwa ili kuondokana na maambukizi ya virusi vya Corona nchini.” Amesema

  • Baadhi ya wadau wakifuatilia hoja mbalimbali katika kikao kilichowakutanisha Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii kwa lengo la kuandaa ujumbe utakaowalenga wazazi kuwaelimisha watoto jinsi ya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona.

Categories

  • News and Events41
  • Conferences4
  • Reports and Publications11
  • success stories 2

Other Posts

  • Sep 06, 25 Call for Consultancy on Assessment of ECD Public Expenditure Review in the Implementation of NM-ECDP I (2021/2022-2025/2026)
  • Aug 25, 25 CALL FOR APPLICATION FOR   CIVIL SOCIETY ORGANIZATIONS TO SUPPORT THE ESTABLISHEMENT OF COMMUNITY ECD CENTRES ACROSS 15 REGIONS OF TANZANIA MAINLAND
  • Jul 23, 25 Tanzania Early Childhood Development Network’s (TECDEN) participation in the Kenya’s 6th National ECD Stakeholders’ Conference. 
  • Jul 21, 25 Tanzania Vision 2050: Placing Early Childhood Development at the Heart of National Transformation
  • Jun 17, 25 COMMEMORATION OF THE DAY OF THE AFICAN CHIL (DAC) 2025

Facebook

Tanzania Early Childhood Development Network (TECDEN)

Our Address

  • Area D-Mlimwa East Plot Number 30 Block K, Dodoma,
  • info@tecden.or.tz
  • +255 755 446 540
  • +255 755 446 540

Quick Links

  • Who We Are
  • What We Do
  • Our Team
  • Our Members
  • Our Partners
  • News & Events
  • Publications
  • Photo Gallery
  • Video Gallery
  • Contact Us
  • Our Locations
  • Privacy Policy

Follow Us

+255 755 446 540

By subscribing to our mailing list you will get the latest news from us.

REQUEST WITH ONLINE FORM

Whats New

  • Call for Consultancy on Assessment of ECD Public Expenditure Review in the Implementation of NM-ECDP I (2021/2022-2025/2026)
  • CALL FOR APPLICATION FOR   CIVIL SOCIETY ORGANIZATIONS TO SUPPORT THE ESTABLISHEMENT OF COMMUNITY ECD CENTRES ACROSS 15 REGIONS OF TANZANIA MAINLAND
  • Tanzania Early Childhood Development Network’s (TECDEN) participation in the Kenya’s 6th National ECD Stakeholders’ Conference. 
  • Tanzania Vision 2050: Placing Early Childhood Development at the Heart of National Transformation
  • COMMEMORATION OF THE DAY OF THE AFICAN CHIL (DAC) 2025
Copyright © 2025 - Tanzania Early Childhood Development Network (TECDEN)